Home » » TUME YAUNDWA MGOGORO WA ARDHI NDARAKWAI

TUME YAUNDWA MGOGORO WA ARDHI NDARAKWAI

SERIKALI imeunda Tume ya Maridhiano itakayoshughulikia chanzo cha mgogoro baina ya mwekezaji wa Ndarakwai na wafugaji wa kimasai walivamia na kuchoma moto nyumba 16 katika shamba la mwekezaji huyo mwezi uliopita.
Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu alipokutana na kamati za ulinzi na usalama za mikoa ya Arusha na Kilimanjaro, alisema namna pekee ya kupata ufumbuzi wa tatizo hilo ni mazungumzo kupitia tume ambayo itaishauri serikali ili ichukue hatua zaidi.
“Naomba tusitoe mwanya kwa tatizo hili kuendelea, lengo la serikali ni kuhakikisha inalipatia ufumbuzi haraka ili kila mmoja aishi kwa amani bila machafuko,” alisema waziri huyo.
Alisema serikali itaendelea kuthamini michango ya wawekezaji wa ndani na nje waliopo nchini huku akitoa maazimio kwa tume hiyo yatakayoleta suluhisho kwa pande.
Miongoni mwa maazimio hayo ni kujua watu walioshiriki kusababisha athari za uharibifu wa mali za mwekezaji huyo na uhalali wa eneo hilo na
kuondoa migogoro inazojitokeza hifadhini.
Novemba 14 mwaka huu, shamba la kampuni ya Tanganyika Film and Safari, mali ya Peter Jones lilivamiwa ambapo magari tisa na nyumba 16 vyenye thamani ya sh bilioni 1.7 viliichomwa moto na wafugaji wa kimasai wakigombania malisho ya mifugo
  Chanzo:Tanzania Daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa