Home » » WANAWAKE WAFUGAJI WAANDAMANA KUPINGA WATENDAJI KUUZA ARDHI.

WANAWAKE WAFUGAJI WAANDAMANA KUPINGA WATENDAJI KUUZA ARDHI.

Zaidi ya wanawake elfu moja kutoka jamii ya kifugaji katika kata ya oljoro namba tano wilayani Simanjiro wamefanya maandamano makubwa ya kuishinikiza serikali iwachukulie hatau watendaji wa kata na kijiji cha namba tano wanaodaiwa kuuza kinyemera zaidi ya hekari elfu thelasini na tano za ardhi ya kijiji na kusababisha mgogoro wa ardhi kati ya wakulima na wafugaji.
Wanawake hao ambao wameandamana hadi katika eneo linalodaiwa kuuzwa na kuwa kiwakilisha kilio chao kwa serikali kupitia mbunge wa jimbo ilo aliyefika katika eneo ilo na kuona maandamano hayo kisha na yeye kuuungana na wanawake hao wakisindikizwa na wenzi wao wamesema wamechoshwa na migogoro na kuitaka serikali kuharakisha kuchukua hatua za kisheria kwa watendaji hao huku diwani wa kata hiyo akiahidi kupambana kufa na kupona katika kutetea ardhi hiyo.
Baada ya kilio cha wananchi hao mbunge wa Simanjiro Christopher Ole Sendeka aliwasimamisha mwenyekiti wa kijiji na mtendaji wake watoe maelezo kuhusu ardhi waliyoiuza zoezi liloonekana kuwa gumu baada ya wote kushindwa kutoa maelezo ya kina huku kila mmoja akijaribu kujitetea binafsi bila mafakinio.
Baadae mbunge huyo akatoa tamko la kuchukuliwa hatua watendaji wote waliyo husika kuhujumu zaidi ya hekari elfu thelasini za ardhi ya kijiji na kudai kamwe kitendo hicho hakivumiki

Chanzo:ITV Tanzania

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa