Home » » VYOMBO VYA DOLA TANZANIA VYASHITAKIWA

VYOMBO VYA DOLA TANZANIA VYASHITAKIWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

Vyombo vya  dola vya Tanzania  vimefikishwa mbele ya Mahakama ya Afrika  ya Haki za Binadamu vikilalamikiwa kukiuka  haki za binadamu wakati wa kushughulikia  wananchi.
 
Vyombo hivyo vimeshtakiwa mahakakani hapo na raia watano wa Kenya  waliohukumiwa miaka 30 kwa kosa la wizi wa  kutumia silaha katika benki ya NBC, tawi la Mwanga  Kilimanjaro.
 
Wakili wa watuhumiwa hao, Donald Deya,  aliwaambia  majaji wa mahakama hiyo kuwa   washitakiwa waliteswa, na kupigwa wakati wakiwa chini ya ulinzi na kusababisha wenzao wawili kupoteza maisha.
 
Deya, ambaye ni mtendaji mkuu  wa Umoja  wa Mawakili  Barani  Afrika  (PALU), aliiiambia mahakama kuwa washitakiwa  waliteswa na kupigwa wakati wakiwa chini ya ulinzi wa vyombo vya dola, jambo ambalo ni kinyume cha sheria na kwamba hata  walipolalamika hawakusikilizwa.
 
Wakili Deya aliiambia mahakama hiyo  iliyokuwa  imefurika wasikilizaji iliyokuwa ikiongozwa na Naibu Rais wa Mahakama hiyo, Elisie Tompson  kutoka Nigeria kuwa washitakiwa wakiwa mahabusu taratibu mbali mbali za kisheria zinazohusu uendeshaji wa kesi hio zilikiukwa  na madai yao ya uchelewashaji wa kesi na kuteswa hayakupewa uzito uliostahiki wala hayakufanyiwa uchunguzi.
 
Naye  wakili  wa  serikali, Nkasoi Sarakika,  ameiambia mahakama kuwa, madai ya  watuhumiwa kupigwa na kuteswa hayana ukweli kwani  taratibu zote za haki zao  zilizingatiwa na kuwa vifo vilivyotokea kwa  watuhumiwa  wawili ni "vya kawaida".
 
Jaji  Elisie Thomson  aliahirisha  shauri hilo  ambalo  sasa  linasubiri  hukumu  inayotarajiwa  kutolewa  baada  ya  miezi  mitatu. 
Mahakama  ya Afrika ya haki za  Binadamu  na watu  ilianzishwa mwaka  2006  nchini Adis Ababa  na  makao  yake  makuu  kuhamishiwa   Arusha  mwaka  2007,  hivi sasa imeanza  kuwa   kimbilio  la  baadhi ya wananchi wa Afrika  wanaolalamika kuwa hawatendewi haki na serikali zao, ndani au nje ya mahakama.
 
Rais wa  Mahakama hiyo,  Jaji  Agustino Ramadhani, alisema mahakama hiyo inakabiliwa  na  changamoto  nyingi  ikiwemo ya baadhi ya nchi ambazo ndio ziliounda mahakama hiyo kuchelewa kutoipa ridhaa yao ya masuala ya nchi zao kusikilizwa na mahakama hii.
Baadhi ya nchi hizo, kwa mujibu wa Jaji Ramadhani, ni uhaba  wa fedha  na kusuasua  kwa  baadhi ya nchi kuridhia mikataba  ya kuanzishwa kwake.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa