Home » » CCM YATOA SIKU SABA ILIPWE KODI.

CCM YATOA SIKU SABA ILIPWE KODI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, kimetoa siku saba kwa wapangaji waliopo kwenye vibanda vya maeneo ya chama hicho, kulipa kodi la sivyo, hatua kali zitachukuliwa kwa watakaokaidi agizo hilo.
Akizungumza na gazeti hili jana mara baada ya kumalizika kwa kikao cha Kamati ya Siasa, Katibu wa Itikadi na Uenezi wilaya ya Hai, Fadhili Juma, alisema kikao hicho kimefikia muafaka huo kutokana na kuwapo usumbufu wa ulipaji kodi kwa wafanyabiashara hao.
Alisema wafanyabiashara hao ni wale waliopo eneo la Uwanja wa Sabasaba ambao idadi yao ni 148, na eneo la ofisi za chama hicho wapatao 48, na kubainisha waliolipa kodi ni wafanyabiashara sita tu.
Juma alisema baada ya Kamati ya Siasa kukaa vikao vingi kwa muda mrefu bila mafanikio kwenye suala la ulipaji na kutii masharti ya mikataba iliyopo, hivyo kikao kimetoa agizo kwa wafanyabiashara hao wawe wamelipa kodi wanayotakiwa kulipa kulingana na makubaliano ndani ya siku saba.
Alisema baada ya muda uliotolewa kupita, chama kitatumia watu wenye mamlaka ya kukusanya kodi hizo ili kufanikisha mpango huo na makusudio ya wafanyabiashara wote kulipa kodi.
Alisema kwa sasa ni muda mrefu maeneo ya CCM yametumiwa na watu kufanya biashara zao, lakini chama kimekuwa hakinufaiki kwa chochote hali inayosababisha kushindwa kujiendesha katika ngazi ya wilaya.
Juma aliwataka wafanyabiashara hao kutambua muda wa kubembelezana umekwisha, na maeneo ya chama hicho hayawezi kugeuzwa shamba la bibi ambalo kila mmoja anafanya biashara zake na kujipatia kipato lakini hataki kulipa kodi kwa mhusika.
 CHANZO ; HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Kilimanjaro Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa